«

»

RADI KWA MAKHAWARIJI

WATAHADHARINI MAKHAWARIJI

NDUGU ZENU KATIKA MASJID ALBANI YA ELIMU ZA HADITHI DAR ES SALAAM

 

بسم الله الرحمن الرحيم

         HUU NI UBAINIFU KWA WATU

Kila sifa njema ni zake Allah mwenye kuhimidiwa na swala na salamu ziwe juu ya mtume wetu ﷺ na ahli zake na maswahaba wake na yule mwenye kumfuaata;

Ama baada ya utangulizi huu, hakika miongoni mwa aliyoneemesha Allah juu yetu baada ya neema ya uislamu na sunna ni neema ya kutafuta elimu ya kisheria, elimu ya kitabu na sunna.

Na kwa hakika Allah ametuwepesishia neema nyingi katika Darul hadith iliyopo masjid Albany rahimahullah tunamshukuru Allah juu ya neema hizo.

Amesema Allah mtukufu “Na hamna neema yoyote mliyo nayo isipokuwa inatoka kwa Allah.”[suratun-nahli 53]

Na miongoni mwa hizo neema ni;

  • Kufuata quran na sunna na kuifanyia kazi, ahlu sunna waljamaa wanalingania katika haki na uislamu sahihi ambao quran na sunna vimeuashiria. Na miongoni mwa yanayolinganiwa na Ahlu sunna ni;

  • Kumpwekesha Allah na kumuabudu peke yake, yeye ndiye aliyewaumba waja na akawaumbia wao yote yaliyomo ardhini.

  • Kufuata kitabu na sunna juu ya ufahamu wa wema waliotangulia, na tunataraji Allah aliyetukuka atufishe katika quran na sunna.

  • Kumpwekesha Allah na kumuabudu peke yake, yeye ndiye aliyewaumba waja na akawaumbia wao yote yaliyomo ardhini.

  • Kushikamana na sunna, na tunatahadharisha kutokana na matamanio ya nafsi na makundi ambayo yanasababisha migongano na mipasuko katika dini.

  • Tunalingania kuelekea katika elimu na subira juu ya elimu na kuifanyia kazi elimu sahihi na kuilingania katika elimu hiyo.

  • Tunalingania watu wote kuelekea katika katika haki, hamna kufaulu kwa nyumati zote na kwa watu wakubwa na wadogo, wanaume na wanawake isipokuwa kwa elimu yenye manufaa na matendo mema na kurejea kwenye dini ya mlezi wa mbingu na ardhi.

  • Kutahadharisha kutokana na kutokuwatii viongozi na makundi ya kisiasa ambayo hamna nyuma yake isipokuwa misiba.

  • Na kwa ajili hiyo ni wajibu kukemea yale ambayo wanayoyafanya MAKHAWARIJI(wanaharakati) na DAESH(ISIS) na AL-SHABABU na BOKO HARAMU katika mauaji na kutoka katika twaa ya viongozi na kulipua mabomu na kukatakata viungo vya mwili na kuunguza na haya yote uislamu hauyakiri na wala Allah hayaridhii wala mtume wake na waumini, bali uislamu unawalingania watu kuelekea kwenye haki na upole na amani na imani na unawatoa watu kutoka katika giza na kufru na uadui.

Uislamu unalingania amani na kila chenye kusaidia juu ya hilo, na katika hayo ni kutahadharisha kutokana na makhawariji ambao wameenda kinyume na dalili sahihi zilizo wazi, na miongoni mwazo; Amesema Allah mtukufu ﮊ Enyi mlio amini! Mt’iini Allah, na mt’iini Mtume na wenye madaraka(juu yenu) katika nyinyi. Na mkizozana katika jambo basi lirudisheni kwa Allah na Mtume, ikiwa mnamuamini Allah na Siku ya Mwisho. Hayo ndiyo bora zaidi na ndiyo yenye mwisho ulio mzuriﮋ  Wamesema wafasiri hao wenye madaraka ni wanachuoni na viongozi

Na kutoka kwa Ibn Abbas — kutoka kwa mtume ﷺ amesema, “yeyote atakaechukia kwa kiongozi wake chochote, basi na asubiri kwa hakika mwenye kutoka katika twaa ya kiongozi wake kiasi cha shibri(ni urefu kuanzia kidole gumba mpaka kwenye kidole cha shahada) hufa kifo cha kijinga” Ameipokea Bukhari.

Na kutoka kwa Anas Bin Malik — kutoka kwa mtume ﷺ amesema “Sikilizeni na tiini na hata kama akitawalishwa juu yenu mhabeshi, kichwa chake kama zabibu”. Ameipokea Bukhari

Na kutoka kwa Ibn Masoud — kutoka kwa mtume ﷺ amesema “ kutakuwa baada yangu ***** na mambo mnayoyapinga, wakasema ewe mtume wa Allah unatuamrisha nini? Akasema, “mnatekeleza haki zilizo juu yenu na mnaomba Allah kile kilicho chenu”. Ameipokea Bukhari na Muslim

Na kutoka kwa Anas Bin Malik — anasema; amesema mtume ﷺ kuwaambia maansari, “Hakika nyinyi mtakutana na ***** baada ya umauti wangu, basi subirini mpaka mkutane nami, na eneo lenu la kukutana nami ni katika hodhi”. Ameipokea Bukhari na Muslim.

Na kutoka kwa Abu Huraira — amesema; amesema mtume ﷺ, “ni wajibu juu yako kusikia na kutii, katika hali ya uzito wako na wepesi wako na katika hali ya uchangamfu wako na kuchukia kwako na ***** juu yako”. ameipokea Muslim.

Na kutoka kwa Abi Dhar — amesema; hakika kipenzi changu ﷺ amenihusia nisikie na nitii na hata kama akiwa ni mtumwa mwenye kukatwa ncha za masikio na niswali swala kwa wakati wake, na ukiwakuta watu wameshaswali utakuwa umeuipata swala yako na kama utawakuta hawajaswali itakuwa swala hiyo kwako ni sunna”. ameipokea muslim.

Na kutoka kwa Ummu Huswein ~~~ amesema, “nilihiji pamoja na mtume ﷺ hijjatul wadaa, amesema Ummu Huswein ~~~ akasema mtume wa Allah ﷺmaneno mengi kisha nikamsikia akisema, “Ikiwa atatawalishwa juu yenu mtumwa aliyekatwa masikio, mweusi, anakuongozeni kwa kutumia kitabu cha Allah, basi msikilizeni na mtiini”. Imepokelewa na Muslim.

Na kutoka kwa Abdillah Ibn Umar — kutoka kwa mtume ﷺ amesema, “Kusikia na kutii ni wajibu juu ya mtu muislam katika yale anayoyapenda na yale anayoyachukia muda wa kuwa hajaamrishwa uovu, na pindi akiamrishwa uovu basi hakuna kusikia wala kutii.” Ameipokea Bukhari na Muslim.

Na utiifu ni katika wema, kutoka kwa Ally — hakika mtume ﷺ amesema, “Hakuna utiifu katika maovu, hakika si vinginevyo utiifu ni katika wema”. Ameipokea Bukhari na Muslim

Na kutoka kwa Abu Huraira — hakika yeye amemsikia mtume ﷺ akisema, hakika si vinginevyo kiongonzi ni ngao, kunapiganwa nyuma yake na kunakingwa kwa kumtumia yeye, i akiamrisha kumcha Allah na akafanya uadilifu, hakika ana ujira kwa hilo, na ikiwa atasema yasiyokuwa hayo hakika juu yake madhambi yake. Ameipokea Bukhari na Muslim

Na mwenye kumpa kiongozi mkono wa utiifu na akampa mkono wake na matunda ya moyo wake basi na amtii akiweza ikiwa atakuja mwingine kumpokonya utawala basi ikatine shingo ya huyo mwingine. Ameipokea Muslim

Na kutoka kwa abu huraira,kutoka,kwa mtume ﷺ amesema “Mwenye kutoka katika twaa na akafarikisha jamaa,kisha akafa basi atakuwa amekufa kifo cha kijinga,na mwenye kupigana chini ya bendera ya upofu,anakasirika kwa ajili ya kundi au analingania kuelekea kwenye kundi au ananusuru kundi kisha akauliwa,basi kuuliwa kwake ni kwa kijinga ,na atakaetoka juu ya umma wangu,anawapiga wema wake na waovu wake wala hatofautishi baina ya waumini wake na wala hatimizi ahadi ya mwenye ahadi,basi [huyo] si katika mimi na wala mimi si katika yeye”Ameipokea Muslim na kwa mfano wake kutoka kwa Jun-dub ameipokea Muslim.

Na kutoka kwa Ibn Umar amesema,nimemsikia mtume ﷺ anasema “Mwenye kuondoa mkono katika twaa atakutana na Allah siku ya qiyama hali ya kuwa hana hoja,na mwenye kufa na hali ya kuwa hamna katika shingo yake baia[kiapo cha utiifu] basi atakuwa amekufa kifo cha kijinga”Ameipokea Muslim

Na kutoka kwa Afajah amesema,nimemsikia mtume ﷺ anasema “kwa hakika patakuwepo misiba na misiba basi mwenye kutaka kufarikisha huu umma hali ya kuwa uko pamoja mpigeni kwa upanga vyovyote atakavyokuwa.Ameipokea Muslim.

Na kutoka kwa Abi Said Al Khudriy amesema amesema mtume ﷺ”Pindi watakapopewa baia[kiapo cha utiifu] makhalifa wawili basi muueni mmoja katika wao”Ameipokea Muslim

Na kutoka kwa Ummu Salamah hakika mtume ﷺamesema “Watakuwepo viongozi mtakiri na mtapinga,mwenye kukiri kwa hakika atakuwa amejiepusha na mwenye kupinga atakuwa amesalimika,lakini mwenye kuridhia na kufuata[hata jiepusha wala hato salimika],wakasema[maswahaba] Je tusiwapige,akasema mtume ﷺ hapana msiwapige muda wa kuwa wanaswali” Ameipokea Muslim

Kutoka kwa Auf Ibn Malik,kutoka kwa mtume ﷺ amesema”Wabora wa viongozi wenu ni wale mnaowapenda na wao wanawapendeni na mnawasalia wao na wao wanawasalieni* na wabaya wa viongozi wenu ni wale mnaowachukia na wao wanawachukieni na nyinyi mnawalaani na wao wanakulaanini, pakasemwa ewe mtume wa Allah Je tusiwaondoe kwa upanga akasema hapana muda wa kuwa wamesimamisha kwenu nyinyi swala.Na mtakapoona kwa viongozi wenu chochote mnachokichukia basi chukieni tendo lake na wala msitoe mkono kutoka katika twaa” Ameipokea Muslim,

Na kutoka kwa Muawiya amesema,amesema mtume ﷺ”Mwenye kufa bila ya imamu atakuwa amekufa kifo cha kijinga”Ameipokea imamu Ahmad na ameisahihisha imamu Al wadiy Allah amrehemu

Na kutoka kwa Zaid Ibn Thabit nimemsikia mtume wa Allah ﷺ anasema “Amemng’arisha Allah mtu aliyesikia kutoka kwetu hadithi kisha akaihifadhi mpaka akamfikishia hadithi hiyo mwingine,kwa hakika huenda mbebaji wa fik-hi si fakihi na huenda mbebaji wa fiq-hi huibeba kuipeleka kwa yule ambaye ana fiq-hi zaidi yake, sifa tatu,***moyo wa muislamu kamwe:kutakasa matendo kwa ajili ya Allah na kuwanasihi viongozi,na kulazimiana na jamaa,hakika daawa yao inazunguka kutokea nyuma yao,na akasema mtume ﷺ”Mwenye kuwa kusudio lake ni akhera Allah hukusanya jambo lake na hujalia utajiri wa mtu huyo kuwa katika moyo chake na humjia dunia mtu huyo hali ya kuwa ni dhalili,na mwenye kuwa kusudio lake ni dunia Allah hufarikisha juu yake jambo lake na hujalia ufakiri wa mtu huyo baina ya macho yake na hakitomjia katika dunia isipokuwa kile alichoandikiwa.”Ameipokea Ahmad na ameisahihisha Al wadiy

Na kutoka kwa Abu Umama amesema nimemsikia mtume wa Allah ﷺ akihutubia katika hijatul wadaa na akasema “ Mcheni Allah mlezi wenu na swalini [swala] tano zenu,na fungeni mwezi wenu na tekelezeni zaka ya mali zenu na watiini mwenye jambo lenu mtaingia pepo ya mlezi wenu”Ameipokea Bukhari na Muslim

Na kutoka kwa Abi Dharri amesema nilisema ewe mjumbe wa Allah hivi kwa nini usinitawalishe   ,amesema abi Dharri akapiga mtume ﷺ kwa mkono wake juu ya bega langu kisha akasema ewe Abu Dharri hakika wewe ni dhaifu na hakika uongozi ni amana na hakika uongozi huo siku ya qiyama ni udhalili na majuto ispokuwa kwa yule aliyeuchukua kwa haki yake na akatimiza lile lililokuwa juu yake katika utawala huo” Ameipokea Muslim

Amesema imamu Ahmad “Lau tungekuwa sisi tuna uombezi wenye kukubaliwa tungeomba kwa uombezi huo kuwaombea viongozi”[Majmuul fatawa na Kushaful qunnai]

NA KILA SIFA NJEMA ZINAMSTAHIKI ALLAH MLEZI WA VIUMBE VYOTE

                             KITABU NA SUNNA JUU YA UFAHAMU WA WATU WEMA       

أضف تعليقاً

لن يتم نشر عنوان بريدك الإلكتروني. الحقول الإلزامية مشار إليها بـ *

يمكنك استخدام هذه HTML الدلالات والميزات: