«

»

BAIQUNIYA

BAIQUNIYA

أبدأُ بالحمدِ مُصَلِّياً عَلَى

أبدأُ بالحمدِ مُصَلِّياً عَلَى

مُحَمَّدٍ خَيْرِ نبيْ أُرسلا

Ninaaza kwa kuhimidi hali ya kumswalia Muhamad, nabii mbora aliyetumwa

وذِي من أقْسَامِ الحَدِيثِ عِدَّهْ

وَكُلُّ واحد أتى وحدَّه

Na hivi ni miongoni mwa vigawanyo vya hadithi vingi na kila kimoja kimekuja na maana yake.

أوَّلُها الصَّحِيحُ وَهْوَ مَا اتَّصل

إسْنَادُهُ وَلَمْ يَشُذَّ أَوْ يُعَلْ

Kigawanyo cha kwanza ni sahihi nayo ni ile ambayo imeunganika, sanadi yake na haikuwa shadha wala

Haikutiliwa dosari

يَرْوِيهِ عَدْلٌ ضَابِطٌ عَنْ مِثْلِه

مُعْتَمَدٌ فِي ضَبْطِهِ وَنَقْلِه

Anaipokea mwadilifu mwenye kudhibiti kutoka kwa mfano wake, mwenye kutegemewa katika udhibiti

Wake na unukuzi wake

والَحسَنُ المعروفُ طُرْقاً وَغَدَتْ

رِجَالُهُ لاَ كالصّحيحِ اشْتَهَرَتْ

Na Hasani ni ile yenye kujulikana njia zake na wakawa, wapokezi wake si kama wa pokezi wa hadithi

Sahihi imekuwa mashuhuru

وكُلُّ مَا عَنْ رُتْبَةِ الحسن قصـر

فهو الضعيف وَهْوَ أَقْسَاماً كُثُرْ

Na kila ile ambayo imepunguwa kutoka katika daraja ya hadithi hasani, basi hiyo ni dhaifu nayo ni

Vigawanyo vingi

وَمَا أُضيفَ لَلنَّبِي المَرْفُوعُ

وَمَا لِتَابِعٍ هو المقطوع

Na ile hadithi iliyoegemizwa kwa Mtume ni marufuu na na iliyoegemezwa kwa Tabiiy ni Maqtwuu

والُمسنَدُ الُمتَّصِلُ الإسنادِ مِنْ

رَاوِيهِ حَتَّى المُصْطَفَى وَلَمْ يَبِنْ

Na hadithi musinadi ni ile ambayo imeunganika sanadi yake kuanzia, kwa mpokezi mpaka mustapha

(Mtumeﷺ) na haikuachana.

وَمَا بِسَمْعِ كُلِّ رَاوٍ يَتَّصِل

إسْنَادُهُ لِلْمُصْطَفَى فَالْمُتَّصِل

Na hadithi ambayo imeunganika sanadi yake kwa kusikia kila mpokezi kutoka kwa mpokezi mwingine

Mpaka kwa mustapha basi hiyo ni mutaswil.

مُسَلْسَلٌ قُلْ مَا عَلَى وَصْفٍ أَتَى

مِثْلُ أَمَا وَاللهِ أنْبأنِي الْفَتَى

Musalsal sema ni ile ambayo umekuja juu ya sifa fulani mfano ama namuapia Allah ameniambia

Mimi Kijana

كذَاكَ قَدْ حَدَّثَنِيهِ قَائما

أَوْ بَعْدَ أَنْ حَدَّثَنِي تَبَسَّمَا

Hivyo hivyo kama kusema amenisimulia mimi hadithi hii hali ya kuwa kasimama au baada ya

Kunisimulia alitabasamu.

عَزِيزُ مَرْوِي اثْنَيْنِ أوْ ثَلاَثَهْ

مَشْهُورُ مَرْوِي فوْقَ مَا ثَلاثهْ

Hadithi Azizi ni ile ambayo imepokelewa na wawili au watatu na hadithi mashuhur ni ile iliyopokelewa

Na watu zaidi ya watatu.

مَعَنْعَنٌ كَعَن سَعِيدٍ عَنْ كَرَمْ

وَمُبْهَمٌ مَا فِيهِ رَاوٍ لَمْ يُسَمْ

Hadithi muan,an ni ile ambayo imepokelewa kwa kutumi lafdh iya ANI kama vile ANI SAIDI(kutoka kwa

Said)ANI KARAM(kutoka kwa karam) na hadithi mubhamu ni ile ambayo ndani yake kuna mpokezi hakutajwa jina lake.

وَكُلُّ مَا قَلَّتْ رِجَالُهُ عَلاَ

وَضِدُهُ ذاك الذي قد نَزَلا

Na kila Isinaad ambayo wamepunguwa wapokezi wake inakuwa ni Isinad iliyo juu na kinyume chake

Hiyo ndiyo ambayo kwahakika inakuwa chini.

ومَا أضَفْتَهُ إِلَى الأَصْحَابِ مِنْ

قَوْلٍ وفعل فهو مَوْقُوفٌ زُكنْ

Na ile ambayo imeegemezwa kwa maswahaba miongoni mwa kauli au kitendo basi hiyo ni Mauquuf

Imefahamika.

وَمُرْسلٌ مِنْهُ الصِّحَابِيُّ سَقَطْ

وَقُلْ غَرِيبٌ مَا رَوَى رَاوٍ فَقَط

Na hadithi Mursal ni ile ambayo ameanguka ndani ya sanadi yake swahaba, na sema hadithi garibu

Ni ile ambayo meipokea mpokezi mmoja tu.

والُمعْضَلُ الساقِط مِنه اثنانِ

وما أتى مُدلساً نَوعانِ

Na hadithi Muudhwal ile ambayo wameanguka ndani ya sanadi yake wawili, na ile hadithi

Ambayo imekuja hali ya kuwa ni Mudalas iko aina mbili

الأَوَّلُ: الاسْقَاطُ لِلشَّيْخِ وَأَنْ

الأَوَّلُ: الاسْقَاطُ لِلشَّيْخِ وَأَنْ

ينقلُ عَمَّنْ فَوْقَهُ بِعَنْ وَأَنْ

Ya mwanzo ni mpokezi kumuangusha shekhe wake na, akanuu kwa aliye juu ya shekhe wake kwa

Kutumia lafudhi ya a’ni na ani.

والثَّانِ: لاَ يُسْقِطُهُ لَكِنْ يَصِفْ

أَوْصَافَهُ بِمَا بِهِ لاَ ينعرف

Na aina ya pili hamuangushi lakini anamusifu, kwa sifa ambazo hawezi kufahamika.

وما يخلف ثِقَةٌ بِهِ الَملأ

فالشاذُّ والَمقْلُوبُ قِسْمَانِ تَلا

Na ile hadith ambayo anakhalifu ndani yake mtu thiqa watu walio bora kuliko yeye, basi hiyo ni shadha

Na hadithi Maqulubu ni vigawanyo viwili vyenye kufuatana.

إبْدَالُ رَاوٍ مَا بِرَاوٍ قِسْمُ

وَقَلْبُ إسْنَادٍ لمَتْنٍ قِسْمُ

Kubadilisha mpokezi kwa mpokezi ni kiwanganyo na kubadilisha sanadi ya matini nyingine hiki ni

kigawanyo kingine

والفَردُ مَا قَيَّدْتَهُ بِثِقةِ

أَوْ جَمْعٍ أوْ قَصـْرٍ عَلَى روايةِ

Na fardu ni ile ambayo umeifungamanisha kwa thiqa, au kundi kutoka katika mji fulani au ########

ومَا بعِلَّةٍ غُمُوضٍ أَوْ خَفَا

مُعَلَّلٌ عِنْدَهُمُ قَدْ عُرِفَا

Na hadithi ambayo ina lla iliyofichikana sana au kidogo, basi hadithi hiyo ni muali(yenye ila ) kwao wao

(watu wa hadithi) kwa hakika imefahamika

وذُو اخْتِلافِ سَنَدٍ أَوْ مَتْنِ

مُضْطَرِبٌ عِنْدَ أُهَيْلِ الْفَنِّ

Na hadithi ambayo ina ikhitilafu nyingi za kisanadi na kimatini, ni Mutwalb kwa watu wa fani ya

Mstwalaha

والُمدْرَجَاتُ فِي الحديثِ مَا أَتَت

مِنْ بَعْض أَلْفَاظِ الرُّوَاةِ اتَّصَلَتْ

Na mudaraji katika hadithi ni zile ambazo zimekuja kutoka katika baadhi ya lafudhi za wapokezi

Ambazo zimeunganika na hadithi.

ومَا رَوى كُلُّ قَرِينٍ عَنْ أَخِهْ

مُدّبَّجٌ فَأَعْرِفْهُ حَقًّا وانْتَخهْ

Na ile waliyoipokea watu wa karini moja kutoka kwa ndugu yake ni Mudabaji ifahamu ukweli wa

kuifahamu

مُتَّفِقٌ لَفْظاً وَخَطاً مُتَّفِقْ

وضِدُّهُ فِيمَا ذَكَرْنَا المُفْتَرِقْ

Na ile ambayo yamefikiana majina ya wapokezi kilafudhi na kimaandishi ni Mutafiq, na kinyume

chake kwa yale tuliyoyataja ni Muftarq

مُؤْتَلِفٌ مُتَّقِقُ الخَطِّ فَقَطْ

وَضِدُّهُ مُخْتَلِفُ فَاخْشَ الْغَلَطْ

Muttalfu ni ile ambayo yameafikiana majina ya wapokezi kimaandishi tu, na kinyume chake ni

mukhtal basi ogopa kukosea

وَالمُنْكَرُ الْفَرْدُ بِهِ رَاوٍ غَدَا

تَعْدِيلُهُ لاَ يْحمِلُ التَّفَرُّدَا

Na munkar ni ile ambayo amepwekeka nayo mpokezi, ambaye kumekuwa kumuadilisha kwake

Hakubebi kupwekea nayo

مَتْرُوكُهُ مَا وَاحِدٌ بِهِ انْفَرَدْ

وَأَجْمَعُوا لِضَعْفِهِ فَهْوَ كَرَدْ

Hadithi matruku ni ile ambayo kapwekeka nayo mtu mmoja nawamekubalia wanachuoni

kwa udhaifu wake basi hadithi hii ni kama yenye kurudishwa

وَالكَذِبُ المُخْتَلَقُ المَصْنُوعُ

وَالكَذِبُ المُخْتَلَقُ المَصْنُوعُ

عَلَى النَّبِي فَذلِكَ الموْضوعُ

Na uongo wenye kuzushwa wenye kutengenezwa juu ya Nabiyﷺ basi hiyo ndiyo hadithi Maudhwuu

وَقَدْ أَتَتْ كَالجَوْهَرِ المَكْنُونِ

سَمَّيْتُهَا مَنْظُومَةَ البَيْقُوني

Na kwa hakika umekuja utenzi huu kama johari yenye kuhifadhiwa nimeuita mandhumat lbayquniy

فَوْقَ الثَّلاثيَن بأرْبَعٍ أتَت

أقْسامُهَا تَمَّتْ بِخَيْرٍ خُتِمَتْ

Imekuja na beti thelathini na nne vigawanyo nyake vimekamilika kwa kher na vimekhitimishwa

أضف تعليقاً

لن يتم نشر عنوان بريدك الإلكتروني. الحقول الإلزامية مشار إليها بـ *

يمكنك استخدام هذه HTML الدلالات والميزات: